エピソード

  • AI, Ibada na Kanisa: A Conversation with Pastor Delphinus Rwegasira
    2026/07/04

    Send us Fan Mail

    Katika episode hii ya Tikvah Podcast, tunakaa na Pastor Del kuzungumza kuhusu Artificial Intelligence na nafasi yake ndani ya Kanisa.

    Je, AI inaweza kutumika kama tool kwenye worship, teaching, na Christian content creation? Au Kanisa linapaswa kuwa makini zaidi?

    This conversation is about wisdom, discernment, biblical truth, and keeping Christ at the center in a fast-changing world.

    AI inaweza kuwa tool, but Christ remains the center.

    続きを読む 一部表示
    1 時間 8 分
  • AI na Ubunifu wa Injili | Je, AI Inaua Creativity au Inaiinua? | Ft. Innocent Mwagilo
    2026/06/27

    Send us Fan Mail

    Katika sehemu ya kwanza ya mfululizo wetu kuhusu AI na Ubunifu wa Injili, tunazungumza na Innocent Mwagilo — Music Producer, Songwriter na Sound Engineer.

    Katika mazungumzo haya tunachunguza namna Artificial Intelligence (AI) inavyoendelea kubadilisha music production na ubunifu kwa ujumla. Je, AI ni tool nyingine tu kama tulivyozoea kutumia studio software, au imeanza kuchukua nafasi ya creativity ya mwanadamu?

    Hili si mjadala wa kupinga au kuunga mkono AI.

    Ni mazungumzo ya kutafuta hekima, kuelewa mabadiliko yanayotokea, na kujiuliza jinsi Wakristo wanavyoweza kuitumia teknolojia kwa namna inayomheshimu Mungu.

    🎙️ Guest: Innocent Mwagilo
    Music Producer | Songwriter | Sound Engineer

    Karibu Tikvah Podcast.

    続きを読む 一部表示
    42 分
  • Yusufu: Kivuli cha Kristo
    2026/06/21

    Send us Fan Mail

    Simulizi la Yusufu siyo tu hadithi ya kutoka gerezani kwenda ikulu. Ni picha inayotuelekeza kwa Kristo.

    Yusufu alikuwa mwana aliyependwa na baba yake, akakataliwa na ndugu zake, akauzwa kwa fedha, akateseka bila hatia, na hatimaye akainuliwa ili kuhifadhi uhai wa wengi.

    Kwa namna kubwa zaidi, yote haya yanatuelekeza kwa Yesu Kristo — Mwana mpendwa wa Baba, aliyekataliwa, aliyeteseka, na kupitia mateso yake akaleta wokovu kwa ulimwengu.

    Katika kipindi hiki tunatafakari kwa nini Misri haikuwa nyumbani kwa Yusufu, na kwa nini Mkristo hapaswi kujenga tumaini lake juu ya mafanikio, mamlaka, mali, au nafasi aliyonayo, bali juu ya Kristo na uzima wa milele.

    Karibu kusikiliza Tikvah Podcast.

    続きを読む 一部表示
    45 分
  • Imani Kwa Mungu Au Imani Kwa Mbinu?-Episode 3
    2026/06/08

    Send us Fan Mail

    Katika Episode hii nimefanya mazungmzo na kaka yangu na mwalimu wangu Faith Joel Shimba Kuhusu namna kanisa limejikuta likibobea katika shughuli za kiroho na kusaua kuhusu Mungu

    続きを読む 一部表示
    57 分
  • Uchambuzi wa Nyimbo-Kitabu by Paul Clement
    2026/05/27

    Send us Fan Mail

    Tumejadili kuhusu live record ya wimbo wa Paul Clement Kitabu(Ajabu) wimbo unapatikana kwenye Youtube channel yake Paul Clement pamoja na Digital Platform zote, tumejadili kuhusu ubora wa utunzi ubora na ubora wa video

    Karibu kusikiliza

    続きを読む 一部表示
    20 分
  • Imani Kwa Mungu Au Imani Kwa Mbinu?-Episode 2
    2026/05/27

    Send us Fan Mail

    Katika episode hii tunachunguza namna ambavyo baadhi ya huduma na makanisa ya kizazi hiki yamehamisha watu kutoka kumtafuta Kristo kwenda kushikilia mbinu, ishara, na experiences za kiroho.

    Kutoka matumizi ya mafuta, maji, udongo, vitambaa, prophetic acts, hadi “gymnastics” nyingi za kiroho , tunajiuliza: Je, hizi ni njia zinazotupeleka kwa Mungu, au zimekuwa distraction inayochukua nafasi ya ujumbe wa kweli wa Injili?

    Kupitia mifano ya Yesu Kristo na mitume:

    • Yesu kutumia mate na udongo kumponya kipofu,
    • Kulisha watu 5000 kwa mikate na samaki,
    • Petro kuponya kupitia kivuli chake,
    • Paulo kupitia leso na vitambaa,

    tunagundua jambo moja muhimu:

    Walifanya miujiza, lakini hawakuwahi kujenga huduma zao juu ya miujiza.

    Ujumbe wao ulikuwa mmoja:
    Kuwaleta watu kwa Mungu.

    🎙 Episode hii ni mwaliko wa kurudi kwenye Injili halisi, kumtafuta Kristo kuliko ishara, na kuhakikisha hatupendi “mkate” kuliko “Bread of Life”.

    #ChristianPodcast #SwahiliPodcast #Injili #Faith #JesusChrist #ChristianLife #Truth #RelationshipWithGod

    続きを読む 一部表示
    11 分
  • Imani Kwa Mungu Au Imani Kwa Mbinu?
    2026/05/21

    Send us Fan Mail

    Katika episode hii tunazungumzia tofauti kati ya kumwamini Mungu na kuamini mbinu za kiroho. Mara nyingi waamini tunajikuta tukiegemea sana maombi, kufunga, ibada, na taratibu mbalimbali za kiroho kiasi kwamba tunasahau kuwa vitu hivi vilikusudiwa kutupeleka kwa Mungu — sio kuchukua nafasi ya Mungu mwenyewe.

    Kupitia simulizi la Musa na mwamba, pamoja na mafundisho ya Yesu kuhusu mapokeo, tunatafakari namna ambavyo mbinu zinaweza kuwa muhimu kuliko uhusiano wa kweli na Mungu.

    Je, bado tunamtafuta Mungu… au tumebaki kushikilia mifumo?

    🎙 Mada hii ni mwaliko wa kurudi kwenye imani ya kweli, ushirika wa kweli, na kumtumaini Mungu zaidi ya tulivyozoea kufanya mambo ya kiroho.

    #Faith #ChristianPodcast #Imani #RelationshipWithGod #ChristianLife #Jesus #SwahiliPodcast

    続きを読む 一部表示
    11 分