『Neno la Leo』のカバーアート

Neno la Leo

Neno la Leo

著者: Neno la Leo 255
無料で聴く

Hii ndiyo siku aliyoifanya Bwana (Zaburi 118:24). Anza siku mpya ya Yesu kwa kusiliza na kutafakari nasi “Neno la Leo” kila siku kwa lugha ya Kiswahili.

Neno la Leo 255
キリスト教 スピリチュアリティ 聖職・福音主義
エピソード
  • Mungu Akifungua Mlango, Atakukuta Uko Tayari?
    2026/09/04

    🎙️ Leo kwenye Neno la Leo

    Leo kupitia 1 Samweli 16:18 tunaendelea na simulizi ya Daudi. Jana tulimwona akipakwa mafuta lakini bado hakwenda moja kwa moja kuwa mfalme. Leo tunasikia mtu akimwelezea kwa Sauli: Daudi anajua kupiga kinubi, ni shujaa, ana busara katika kusema na zaidi ya yote, Bwana yu pamoja naye.

    Jambo la kuvutia ni kwamba sifa hizi hazikuanza kujengwa siku ambayo nafasi ya kwenda ikulu ilifunguka. Daudi alikuwa ameanza kujiandaa wakati hakuna aliyekuwa akimtazama.

    Alijifunza kupiga kinubi bila kujua kwamba siku moja muziki huo ungemfungulia mlango wa ikulu. Alijifunza kuwa mwaminifu akichunga kondoo bila kujua kwamba ujasiri aliokuwa akiujenga huko malishoni ungehitajika katika hatua kubwa zaidi za maisha yake.

    Fursa ilipofika, maandalizi yalikuwa yameanza zamani.

    Nasi mara nyingi tunamwomba Mungu atufungulie milango. Tunaomba kazi, biashara ikue, huduma ipanuke, tupate cheo au nafasi kubwa zaidi. Lakini pamoja na kuomba mlango ufunguke, kuna swali jingine tunalopaswa kujiuliza: Mlango ukifunguka leo, je, niko tayari?

    Usisubiri nafasi ndipo uanze kujenga uwezo. Usisubiri watu wakutambue ndipo uanze kujenga tabia. Jenga leo kile ambacho kesho yako itahitaji. Tumia vizuri kipindi ambacho hakuna anayekuona kwa sababu huenda Mungu anakitumia kukuandaa kwa nafasi ambayo bado hujaiona.

    Lakini kati ya sifa zote za Daudi, Biblia inataja moja ambayo ni kubwa kuliko zote: “Bwana yu pamoja naye.” Tunaweza kujenga ujuzi, uzoefu na uwezo lakini maandalizi yetu makubwa zaidi ni kujifunza kutembea pamoja na Mungu.

    Kwa hiyo usiombe tu, “Bwana, nifungulie mlango.” Omba pia, “Bwana, nitengeneze ili mlango utakapofunguka, niwe tayari.”

    Karibu tusikilize, tutafakari na kujifunza pamoja. 🙏📖✨

    続きを読む 一部表示
    33 分
  • Ruhusu Mungu Akutengeneze.
    2026/09/03

    🎙️ Leo kwenye Neno la Leo

    Leo kupitia 1 Samweli 16:13 tunaendelea na simulizi ya Daudi. Jana tulimwacha malishoni, mahali ambapo watu hawakumfikiria lakini Mungu alikuwa amemwona. Leo anaitwa nyumbani na Mungu anamwambia Samweli, “Ondoka, umtie mafuta, maana huyu ndiye.” Daudi anapakwa mafuta katikati ya ndugu zake na Roho wa Bwana anakuja juu yake.

    Lakini jambo la kushangaza ni hili: Daudi alipakwa mafuta kuwa mfalme lakini hakwenda moja kwa moja kukalia kiti cha enzi.

    Alikuwa amechaguliwa lakini bado alikuwa na safari. Kulikuwa na tofauti kati ya kusudi alilopewa na utayari wa kulibeba.

    Nasi tunaweza kufanya kosa la kutaka kila kitu kitokee mara tu tunapoanza kuona kusudi la Mungu katika maisha yetu. Tunapata ndoto, maono, kipawa au nafasi fulani na tunataka jukwaa mara moja. Lakini Mungu anaweza kukuita leo na bado akatumia muda kukufundisha, kukukomaza na kuandaa tabia yako kwa kile anachotaka kukukabidhi kesho.

    Usikimbilie jukwaa kwa sababu tu umeona kusudi. Ruhusu Mungu akutengeneze.

    Daudi alipakwa mafuta kabla taifa halijamtambua. Mungu alikuwa ameona ndani yake kile ambacho wengine bado hawajakiona. Kwa hiyo kama watu bado hawaoni kile Mungu anaweka ndani yako, usiwe na haraka ya kujithibitisha. Endelea kuwa mwaminifu katika hatua uliyo nayo sasa.

    Swali si tu, “Je, Mungu amenichagua?” Swali jingine muhimu ni, “Je, ninamruhusu Mungu aniandae kwa kile alichonichagulia?”

    Kwa sababu wakati wako utakapofika, hutahitaji tu nafasi. Utahitaji uwezo na tabia ya kubeba kile ambacho Mungu amekukabidhi.

    Karibu tusikilize, tutafakari na kujifunza pamoja. 🙏📖✨

    続きを読む 一部表示
    19 分
  • Usidharau Mahali Ulipo Sasa!
    2026/09/02

    🎙️ Leo kwenye Neno la Leo

    Leo kupitia 1 Samweli 16:11 tunaendelea na safari tuliyoanza jana. Samweli amefika nyumbani kwa Yese kumpaka mafuta mfalme mpya wa Israeli. Wana wa Yese wanapita mbele yake mmoja baada ya mwingine lakini Mungu hamchagui hata mmoja. Hatimaye Samweli anauliza, “Je, hawa ndio wanao wote?”

    Ndipo tunagundua kwamba kuna mmoja ambaye hata hakuitwa. Daudi yuko malishoni akichunga kondoo.

    Fikiria hilo. Mfalme ajaye wa Israeli yuko shambani wakati mkutano unaohusu maisha yake unaendelea nyumbani. Hakualikwa, hakutajwa mwanzo na hakuna aliyedhani kwamba ndiye ambaye Mungu alikuwa akimtafuta. Lakini kutokualikwa na watu hakumaanishi alikuwa amesahaulika na Mungu.

    Na huenda hilo ndilo Neno la leo kwa mtu fulani. Unaweza kujisikia kama uko “malishoni” wakati wengine wako mbele ya Samweli. Wengine wanapandishwa vyeo, wanatambuliwa, wanapewa nafasi na wanaonekana kusonga mbele huku wewe ukiendelea kufanya kazi ileile ambayo hakuna anayeshangilia.

    Usidharau mahali ulipo sasa.

    Daudi hakujua kwamba mikono iliyokuwa ikilinda kondoo siku moja ingelinda taifa. Hakujua kwamba mazingira yale ya kawaida yalikuwa sehemu ya maandalizi ya Mungu kwa maisha yake. Mahali ambapo hakuna anayekuona panaweza kuwa mahali ambapo Mungu anakutengeneza.

    Kwa hiyo usidharau kazi ndogo. Usidharau majukumu yasiyoonekana. Usidharau kipindi ambacho hakuna anayekutambua. Endelea kuwa mwaminifu. Mungu anaweza kutumia kile unachofanya leo kukuandaa kwa kile ambacho bado hujakiona.

    Na kumbuka hili: Unaweza kuwa umefichika kwa watu lakini hujafichika kwa Mungu. Watu wanaweza kusahau kukuita lakini Mungu hajakusahau.

    Karibu tusikilize, tutafakari na kujifunza pamoja. 🙏📖✨

    続きを読む 一部表示
    37 分
adbl_web_anon_alc_button_suppression_t1
まだレビューはありません