『Neno la Leo』のカバーアート

Neno la Leo

Neno la Leo

著者: Neno la Leo 255
無料で聴く

Hii ndiyo siku aliyoifanya Bwana (Zaburi 118:24). Anza siku mpya ya Yesu kwa kusiliza na kutafakari nasi “Neno la Leo” kila siku kwa lugha ya Kiswahili.

Neno la Leo 255
キリスト教 スピリチュアリティ 聖職・福音主義
エピソード
  • Mwanzo wa Muujiza Huanzia Katikati ya Ukame
    2026/07/16

    🎙️ Leo kwenye Neno la Leo

    Leo tunaanza simulizi ya Ruthu kupitia Ruthu 1:1. Safari inaanza wakati wa njaa na huzuni, lakini nyuma ya pazia Mungu alikuwa tayari anaandaa mpango wa ukombozi. Kupitia simulizi hii tunajifunza kwamba Mungu mara nyingi huanza kazi yake kubwa pale ambapo sisi tunaona kila kitu kimeharibika. Je, inawezekana kwamba kipindi unachokiita ukame ndicho Mungu anakitumia kuandaa msimu wako mpya?

    続きを読む 一部表示
    14 分
  • Hitimisho la Kitabu cha Waamuzi: Nani Ameketi Kwenye Kiti cha Enzi cha Maisha Yako?
    2026/07/15

    🎙️ Leo kwenye Neno la Leo

    Leo tunahitimisha kitabu cha Waamuzi kupitia Waamuzi 21:25. Baada ya safari ndefu ya kuona ushindi, kuanguka, toba na kurudia makosa yale yale, Biblia inatupa hitimisho moja lenye uzito: “Kila mtu alifanya alivyoona ni vyema machoni pake.” Kupitia hitimisho hili tunajifunza kwamba chanzo cha machafuko ya Israeli hakikuwa ukosefu wa viongozi au nguvu, bali kumwondoa Mungu katika kiti cha enzi cha mioyo yao. Je, ni nani anayeyaongoza maamuzi yako leo, maoni yako mwenyewe, sauti ya dunia au Neno la Mungu?

    Karibu tusikilize, tutafakari na kuhitimisha pamoja safari yetu ya kitabu cha Waamuzi. 🙏📖✨

    続きを読む 一部表示
    13 分
  • Je, Utachagua Kweli au Maslahi ya Kundi Lako?
    2026/07/14

    Leo kwenye Neno la Leo

    Leo tunaendelea na hitimisho la kitabu cha Waamuzi kupitia Waamuzi 20:12–14. Baada ya uovu mkubwa kutendeka huko Gibea, makabila ya Israeli yalitaka haki itendeke. Lakini kabila la Benyamini lilichagua kuwatetea waovu badala ya kusimama upande wa kweli. Kupitia tukio hili tunajifunza kwamba jamii huanza kuporomoka pale ambapo uaminifu kwa familia, kabila, kundi au maslahi binafsi unakuwa mkubwa kuliko utii kwa Mungu na kweli yake. Je, tuko tayari kusimama upande wa haki hata inapogharimu maslahi yetu au ya watu tunaowapenda?

    Karibu tusikilize, tutafakari na kujifunza pamoja. 🙏📖✨

    続きを読む 一部表示
    21 分
adbl_web_anon_alc_button_suppression_t1
まだレビューはありません