『Utii ni Bora Kuliko Dhabihu!』のカバーアート

Utii ni Bora Kuliko Dhabihu!

Utii ni Bora Kuliko Dhabihu!

無料で聴く

ポッドキャストの詳細を見る

🎙️ Leo kwenye Neno la Leo

Leo kupitia 1 Samweli 15:22–23 tunafika katika moja ya nyakati muhimu sana katika maisha ya Sauli. Mungu alikuwa amempa agizo lakini Sauli hakulitekeleza kikamilifu. Alipoulizwa kwa nini, akatoa sababu iliyosikika ya kiroho: baadhi ya vitu vilihifadhiwa ili vitolewe sadaka kwa Bwana. Ndipo Samweli akasema maneno ambayo yameendelea kutukumbusha mpaka leo: “Kutii ni bora kuliko dhabihu.”

Tatizo la Sauli halikuwa kwamba hakumtii Mungu kabisa. Alitii sehemu ya agizo na akaacha sehemu ambayo haikumfaa. Kisha akajaribu kutumia jambo la kidini kuhalalisha kile ambacho Mungu hakumwagiza.

Na hapo ndipo Neno la leo linapotufikia sisi pia. Je, inawezekana nasi tukawa tunamtii Mungu kwa masharti yetu? Tunaweza kwenda kanisani, kuomba, kutoa sadaka, kusoma Neno na kuwahudumia wengine lakini wakati huohuo tukawa tunapuuza jambo ambalo tunajua Mungu anatutaka tulirekebishe. Ibada haiwezi kuwa mbadala wa utiifu.

Swali la leo si tu, “Je, ninamtii Mungu?” Bali ni: “Je, ninamtii Mungu hata pale mapenzi yake yanapopingana na yale ninayotaka?” Kwa sababu utiifu wa kweli hauchagui maagizo yanayotufaa na kuacha yale yanayotugharimu.

Mungu hatutafuti tu kuwa watu wanaofanya mambo yanayoonekana ya kiroho. Anataka mioyo inayoweza kusema, “Bwana, hata kama ni vigumu, nitakutii.”

Karibu tusikilize, tutafakari na kujifunza pamoja. 🙏📖✨

adbl_web_anon_alc_button_suppression_t1
まだレビューはありません