Usidharau Mahali Ulipo Sasa!
カートのアイテムが多すぎます
カートに追加できませんでした。
ウィッシュリストに追加できませんでした。
ほしい物リストの削除に失敗しました。
ポッドキャストのフォローに失敗しました
ポッドキャストのフォロー解除に失敗しました
-
ナレーター:
-
著者:
🎙️ Leo kwenye Neno la Leo
Leo kupitia 1 Samweli 16:11 tunaendelea na safari tuliyoanza jana. Samweli amefika nyumbani kwa Yese kumpaka mafuta mfalme mpya wa Israeli. Wana wa Yese wanapita mbele yake mmoja baada ya mwingine lakini Mungu hamchagui hata mmoja. Hatimaye Samweli anauliza, “Je, hawa ndio wanao wote?”
Ndipo tunagundua kwamba kuna mmoja ambaye hata hakuitwa. Daudi yuko malishoni akichunga kondoo.
Fikiria hilo. Mfalme ajaye wa Israeli yuko shambani wakati mkutano unaohusu maisha yake unaendelea nyumbani. Hakualikwa, hakutajwa mwanzo na hakuna aliyedhani kwamba ndiye ambaye Mungu alikuwa akimtafuta. Lakini kutokualikwa na watu hakumaanishi alikuwa amesahaulika na Mungu.
Na huenda hilo ndilo Neno la leo kwa mtu fulani. Unaweza kujisikia kama uko “malishoni” wakati wengine wako mbele ya Samweli. Wengine wanapandishwa vyeo, wanatambuliwa, wanapewa nafasi na wanaonekana kusonga mbele huku wewe ukiendelea kufanya kazi ileile ambayo hakuna anayeshangilia.
Usidharau mahali ulipo sasa.
Daudi hakujua kwamba mikono iliyokuwa ikilinda kondoo siku moja ingelinda taifa. Hakujua kwamba mazingira yale ya kawaida yalikuwa sehemu ya maandalizi ya Mungu kwa maisha yake. Mahali ambapo hakuna anayekuona panaweza kuwa mahali ambapo Mungu anakutengeneza.
Kwa hiyo usidharau kazi ndogo. Usidharau majukumu yasiyoonekana. Usidharau kipindi ambacho hakuna anayekutambua. Endelea kuwa mwaminifu. Mungu anaweza kutumia kile unachofanya leo kukuandaa kwa kile ambacho bado hujakiona.
Na kumbuka hili: Unaweza kuwa umefichika kwa watu lakini hujafichika kwa Mungu. Watu wanaweza kusahau kukuita lakini Mungu hajakusahau.
Karibu tusikilize, tutafakari na kujifunza pamoja. 🙏📖✨