『Mungu Haangalii Sura, Anaangalia Moyo Wako!』のカバーアート

Mungu Haangalii Sura, Anaangalia Moyo Wako!

Mungu Haangalii Sura, Anaangalia Moyo Wako!

無料で聴く

ポッドキャストの詳細を見る

🎙️ Leo kwenye Neno la Leo

Leo kupitia 1 Samweli 16:7 tunaanza mwezi mpya na hatua mpya katika simulizi ya 1 Samweli. Agosti tuliimaliza na Sauli, mtu aliyeanza vizuri lakini ambaye hatua kwa hatua alianza kuweka maamuzi yake mbele ya utiifu kwa Mungu. Sasa Samweli ametumwa nyumbani kwa Yese kumtafuta mfalme mwingine.

Anapomwona Eliabu, Samweli anavutiwa na kile kinachoonekana kwa macho. Anaonekana kama mtu anayefaa kuwa mfalme. Lakini Mungu anamfundisha jambo ambalo litakuwa msingi wa safari yetu na Daudi: mwanadamu huangalia sura ya nje lakini Bwana huangalia moyo.

Na hapo ndipo tunapoanzia Septemba: moyoni.

Tunaishi katika dunia inayotufundisha kujenga kile watu wanaweza kuona. Muonekano, elimu, cheo, fedha, mafanikio, followers na namna tunavyoonekana mbele za wengine. Lakini Mungu anaona mahali ambapo hakuna mwanadamu anayeweza kuona kikamilifu. Anaona nia zetu, tamaa zetu, sababu zinazotusukuma kufanya tunayofanya na tabia yetu wakati hakuna anayetuangalia.

Hii ndiyo tofauti tutakayoanza kuiona kati ya Sauli na Daudi. Siyo kwamba Daudi alikuwa mkamilifu. Tutakuja kuona makosa yake pia. Lakini Mungu alikuwa akitafuta moyo unaoweza kumrudia, kumsikiliza na kutengenezwa naye.

Kwa hiyo tunapoanza mwezi huu, labda kabla hatujamwomba Mungu abadilishe kazi yetu, biashara yetu, mahusiano yetu au mazingira yetu, tuanze na ombi la ndani zaidi: “Bwana, tengeneza moyo wangu.”

Na swali letu la kwanza la Septemba liwe hili:

Mungu akiangalia moyo wangu leo, anaona nini?

Kwa sababu watu wanaweza kuvutiwa na kile kilicho nje lakini Mungu huanzia ndani.

Karibu tusikilize, tutafakari na kujifunza pamoja. 🙏📖✨

adbl_web_anon_alc_button_suppression_t1
まだレビューはありません