Ruhusu Mungu Akutengeneze.
カートのアイテムが多すぎます
カートに追加できませんでした。
ウィッシュリストに追加できませんでした。
ほしい物リストの削除に失敗しました。
ポッドキャストのフォローに失敗しました
ポッドキャストのフォロー解除に失敗しました
-
ナレーター:
-
著者:
🎙️ Leo kwenye Neno la Leo
Leo kupitia 1 Samweli 16:13 tunaendelea na simulizi ya Daudi. Jana tulimwacha malishoni, mahali ambapo watu hawakumfikiria lakini Mungu alikuwa amemwona. Leo anaitwa nyumbani na Mungu anamwambia Samweli, “Ondoka, umtie mafuta, maana huyu ndiye.” Daudi anapakwa mafuta katikati ya ndugu zake na Roho wa Bwana anakuja juu yake.
Lakini jambo la kushangaza ni hili: Daudi alipakwa mafuta kuwa mfalme lakini hakwenda moja kwa moja kukalia kiti cha enzi.
Alikuwa amechaguliwa lakini bado alikuwa na safari. Kulikuwa na tofauti kati ya kusudi alilopewa na utayari wa kulibeba.
Nasi tunaweza kufanya kosa la kutaka kila kitu kitokee mara tu tunapoanza kuona kusudi la Mungu katika maisha yetu. Tunapata ndoto, maono, kipawa au nafasi fulani na tunataka jukwaa mara moja. Lakini Mungu anaweza kukuita leo na bado akatumia muda kukufundisha, kukukomaza na kuandaa tabia yako kwa kile anachotaka kukukabidhi kesho.
Usikimbilie jukwaa kwa sababu tu umeona kusudi. Ruhusu Mungu akutengeneze.
Daudi alipakwa mafuta kabla taifa halijamtambua. Mungu alikuwa ameona ndani yake kile ambacho wengine bado hawajakiona. Kwa hiyo kama watu bado hawaoni kile Mungu anaweka ndani yako, usiwe na haraka ya kujithibitisha. Endelea kuwa mwaminifu katika hatua uliyo nayo sasa.
Swali si tu, “Je, Mungu amenichagua?” Swali jingine muhimu ni, “Je, ninamruhusu Mungu aniandae kwa kile alichonichagulia?”
Kwa sababu wakati wako utakapofika, hutahitaji tu nafasi. Utahitaji uwezo na tabia ya kubeba kile ambacho Mungu amekukabidhi.
Karibu tusikilize, tutafakari na kujifunza pamoja. 🙏📖✨